HUDUMA YA MTANDAO YAREJESHWA NCHINI UGANDA
Jan 18, 2026
Mtandao umerejeshwa nchini Uganda saa chache baada ya kutangazwa kuwa Yoweri Museveni ameshinda uchaguzi wa Urais.
Serikali ilikuwa imefunga Mtandao siku ya Jumanne, ikisema ilikuwa ni kuzuia kuenea kwa habari potofu na kulinda usalama wa taifa.
Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa imeita hatua hiyo wasiwasi mkubwa.
Ilikuwa ni mara ya pili kwa Mamlaka ya Uganda kufunga mtandao wa nchi hiyo wakati wa Uchaguzi kwa misingi ya usalama.
Kuzima kwa mara ya kwanza kama hii ilikuwa mnamo 2021, na kuathiri zaidi ya watumiaji milioni 10 wanaotumia mtandao.
