Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
UN YASIKITISHWA NA UVAMIZI WA VENEZUELA

UN YASIKITISHWA NA UVAMIZI WA VENEZUELA

 


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema "ana wasiwasi mkubwa" na operesheni ya kijeshi ya Marekani nchini Venezuela, akiongeza kuwa ina "athari za kutia wasiwasi kwa eneo hilo", kulingana na taarifa iliyotolewa na msemaji wa UN.

"Bila kujali hali ilivyo nchini Venezuela, matukio haya ni mfano hatari," inasema taarifa hiyo.

"Katibu Mkuu ameendelea kusisitiza umuhimu wa heshima - kwa wote - kwa sheria za kimataifa, ikiwa ni pamoja na Mkataba wa Umoja wa Mataifa. Ana wasiwasi mkubwa kwamba kanuni za sheria za kimataifa hazijaheshimiwa."

Pia alitoa wito kwa Venezuela kushiriki katika "mazungumzo yenye kujumuisha kila mmoja" kwa kuheshimu haki za binadamu na utawala wa sheria.

Mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa umeitishwa Jumatatu na Colombia kwa usaidizi wa Urusi na China.

Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3