Kwa Habari za kitaifa, Kimataifa, Michezo, Burudani,Uchambuzi na matangazo. Matukio Daima Blog, Ni yetu Sote!
WANANCHI TUMIENI VYANDARUA KUPAMBANA NA MALARIA SIO KUFUGIA KUKU

WANANCHI TUMIENI VYANDARUA KUPAMBANA NA MALARIA SIO KUFUGIA KUKU

 

Na Lilian Kasenene, Morogoro

Matukio DaimaApp 

WANANCHI mkoa wa Morogoro wametakiwa kutumia vyandarua kwa matumizi yaliyokusudiwa na si vinginevyo,ikiwa ni hatua ya kupambana na maambukizi ya ugonjwa wa Malaria.

Morogoro ni kati ya mikoa 10 inayoongoza kwa maambukizi ya wingi wa malaria kwenye mikoa 26 na lengo ni kutika kwenye idadi hiyo.

Mkuu wa mkoa wa Morogoro Adam Malima alisema hayo wakati wa kikao Cha uhamasishaji kwa viongozi kuhusu mpango wa ugawaji wa vyandarua ngazi ya kaya.

"Sasa nakubaliana na angalizo lililowekwa, tukianza kutumia vyandarua hivi kwa mambo mengine ambayo sio makusidio yake tutakuwa hatujatendea haki zoezi zima na Nia nzuri ya Serikali, tutakuwa wakali sana kwenye hili, unapewa chandarua harafu unatumia sivyo hatutaelewana "alisema Rc Malima.

Malima alisisitisa umuhimu wa kila mwananchi kutumia chandarua kwa ajili ya kujikinga na mbu, badala ya kutumia vyandarua hivyo kwa shughuli nyingine ambazo sio lengwa.

Mkuu huyo wa mkoa alisema matumizi yasiyo sahihi ya vyandarua yamekuwa changamoto kwa juhudi za Serikali na wadau katika kutokomeza ugonjwa wa malaria,hivyo viongozi wa umma wanapaswa kuwa mstari wa mbele kutoa elimu kwa jamii juu ya matumizi sahihi ya vyandarua.

"Lazima tuwe na elimu kwa umma ifanyike kwa wote,agizo langu ni kwa Watendaji wote wa umma lazima wawe na Elimu ya kupambana na malaria,na izungumzwe kwenye vikao vyote,"alisema.

Katibu tawala mkoa wa Morogoro Dk Mussa Ali Mussa alisema Sasa ni wakati wa kufanya tafiti za kina ili kubaini maeneo yenye viwango vya juu vya maambukizi ya malaria hatua itakayosaidia kuboresha mikakati ya kuzuia ugonjwa wa malaria.

Dk Ali Mussa alisema Morogoro una uasilia wa Mazingira tofauti hivyo tathimini na tafiti utaenda sambamba eneo husika.

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISENI) idara ya afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Januari Boniventura,alisema  bado kuna changamoto ya baadhi ya wananchi kutumia vyandarua kwa matumizi yasiyo sahihi.

Alisema Matumizi hayo ni pamoja na baadhi ya wananchi kufugia kuku, na kufunika bustani jambo linalohatarisha afya ya jamii.

Mratibu wa Huduma za Malaria mkoa wa Morogoro Dk Wahida Mtiro alisema kitakwimu katika suala la Malaria,wanawake ndio wanaongoza huku wanaume wakionekana kuwa na idadi ndogo kutokana na kutojitokeza kupima.

DK Mtiro alisema kwa takwimu za mwaka 2025 Wanawake ni 75,000 na wanaume ni 60,000 kwa wale waliojitokeza kupima malaria pekee.

Mkoa wa Morogoro unatarajia kupata vyandarua milioni 1.5 kwa kila kaya kwenye Halmashauri saba



Sponsored ads

Mid 1

Mid2

Ad3